Wednesday, November 12, 2014

Hodgson ammwagia sifa kemkem Rooney


Kocha wa England Roy Hodgson amemsifu nahodha wa timu hiyo ya taifa Wayne Rooney kabla hajacheza mechi ya 100 katika michuano ya michuano ya ulaya mwaka 2016, ambapo England itakutana na Slovenia.

Rooney (29), alianza kuichezea timu ya England akiwa na miaka 17 mwaka 2003 na ni mfungaji wa nafasi ya nne akiwa ashatia nyavuni magoli 43.
Rooney ana kadi sita nyekundu, mbili akiwa na England, Hodgson ameeleza. Kazi yake hii imekuwa na vikwazo ya kila namna lakini imemkomaza na kumkuza kiakili.
Akizungumza na Radio 5 ya BBC, Hodgson amesema kuwa Rooney ni mkombozi wa soka la uingereza, huhakikisha kuwa kila mmoja yuko sawa na anaridhika na kuhakikisha kuwa hakuna tatizo ndani ya kikosi.

HABARI MPYA.

Michezo-Mwananchi

Burudani

MwanaspotiSoka